![]() |
| baadhi ya wanajeshi wa USA |
Jenerali Mark Milley, amesema mwanajeshi
mmoja ndiye aliyewafyetulia wenzake risasi hizo karibu na zahanati ya afya ya
kijeshi ya Carl R Darnall iliyoko katika kambi hiyo ya Jeshi.
Watu watatu walifariki kabla ya mwanajeshi
huyo kujipiga risasi na kujiua.
Wanajeshi wapato wanne wanatibiwa majeraha
mabaya ya risasi.
Daktari mkuu wa zahanati hiyo Dakta Glen
Couchman anaelezea majeraha wanayotibu.
''Wote walikuwa na majereha mbalimbali ya
risasi kwenye vifua shingo na tumbo''.
Mauaji katika kambi ya Jeshi Marekani
Waziri wa usalama Chuck Hagel amesema kuwa
uchunguzi tayari umeshaanza kubaini chanzo cha kisa hicho cha pili kuikumba
kambi hii.'
Rais Obama amehuzunishwa sana na tukio hilo
ambalo anasema limetokea katika kambi ambayo inapaswa kuwa salama .
WANAJESHI WAUWAWA MAREKANI

No comments:
Post a Comment